Skip to main content

Bwana Fortunatus Magambo – Mtanzania

Mwenyekiti

Ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi tangu mwaka 2018. Katika nafasi hiyo, mtazamo wake ni kubuni mikakati na sera za Kampuni, kuimarisha uongozi, na kukidhi matakwa ya wanahisa. Hivi sasa Bwana Magambo ni Mkurugenzi wa Mipango na Uwekezaji wa Mfuko wa PSSSF na anauwakilisha Mfuko huo kwenye Bodi. Ni Mjumbe wa Bodi wa Nguru Hills Ranch Ltd, Benki ya Posta na  Ubungo Plaza Ltd. Ana uzoefu kwenye maeneo yafuatayo:-  Utawala, Uongozi, Mashirika, Usimamizi, Utafutaji na usimamizi wa miradi mikubwa na midogo, kuongea lugha mbalimbali, mashirika ya umma na mashirika binafsi. Amewahi kufanya kazi kama  Meneja wa Hazina wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii LAPF. Kupitia uzoefu wake, ameweza kuzisaidia Bodi nyingi kwenye Changamoto ya kifedha na kujiimarisha, kuendesha Biashara kubwa, kusaidia kukuza biashara mpya, na pia ana uwezo wa kuandaa Mpango Mkakakati kwa Maendeleo ya Shirika. Bwana Magambo alipata shahada yake ya kwanza kutoka Hanze University College – Groningen – Uholanzi, Shahada ya Uongozi wa Biashara katika masuala ya Fedha na Uhasibu, na ana shahada ya Uzamivu (Dutch Doctoral Programme – Doctorandus (Drs) - Associate Doctorate and MSc (Economics) – Kitivo cha Uchumi na Uongozi wa Biashara - kutoka Tilburg University - Uholanzi: Julai 2003.

Bwana Nathan Edward Mnyawami – Mtanzania

Mjumbe

Bwana Mnyawami ana Shahada ya Uchumi kutoka Chuo Kikuu cha Makerere, 1993 na Shahada ya Uzamili ya Uchumi kutoka Chuo kikuu cha Dar es Salaam, 2002. Bwana Mnyawami ana uzoefu wa miaka 20 katika kazi.  Kuanzia mwaka 1994 hadi 2002, alikuwa ameajiriwa na Shirika la Maendeleo ya Petroli (TPDC) kama Mtakwimu chini ya Mkurugenzi wa Masoko na Uwekezaji. Oktoba, 2002 hadi 2015 alijiunga na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa Mashirika ya Umma (PPF) kama Mratibu/ Meneja wa Mipango na Utafiti. Alijiunga tena na TPDC mwaka 2015 kama Mkurugenzi wa Mipango na Uwekezaji. Bwana Mnyawami ni mjumbe wa Kamati ya Uwekezaji na amesajiliwa na Chuo cha Wakurugenzi Tanzania (IoDT).

Bi. Magdalene Nelson Enock Mkocha – Mtanzania

Mjumbe

Bi Mkocha ana shahada ya Sayansi katika Kilimo kutoka Chuo Kikuu cha Dar-es-Salaam, 1979, na shahada ya Uzamili ya Sayansi katika Kilimo kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine. 1988. Ana uzoefu wa kufanya kazi wa miaka 37. Kutoka Aprili 1979 hadi Juni 2002 aliajiriwa na Shirika la Kilimo na Chakula (NAFCO). Mwezi Julai 2002 alijiunga na Chama cha wafanyabiashara, wenye Viwanda na Kilimo Tanzania kama Afisa Mwandamizi wa Maendeleo wa TCCIA na Mkurugenzi wa Maendeleo ya Kilimo. Yeye ni mjumbe wa Kamati ya Ukaguzi na Athari za Kampuni. Bi Mkocha ni mjumbe wa Bodi/Kamati zifuatazo:- Baraza la Kazi, Uchumi na Ustawi la Wizara ya Kazi, Bodi ya Nyama Tanzania, Kamati ya Taifa ya Usafi, Mwenyekiti wa Kamati ya Ushauri ya VETA na mjumbe wa Kamati ya Ufundi ya Ushauri ya Bodi ya Sukari Tanzania. Pia amesajiliwa na Chuo cha Wakurugenzi Tanzania (IoDT).

Prof. Lucian Ambrose Msambichaka – Mtanzania

Makamu Mwenyekiti

Prof. Msambichaka ana Shahada ya Kilimo kutoka Chuo Kikuu cha Dar-s- Salaam, Shahada ya Uzamili na Uzamivu kutoka Chuo Kikuu cha   Leipzig Ujerumani. Prof. Msambichaka ni Mjumbe wa Bodi zifuatazo: Jumuiya ya Uchumi ya Kilimo Tanzania, Jumuiya ya Uchumi Tanzania na Utawala na Usimamizi wa Umma katika Jumuiya ya Afrika. Na pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Uwekezaji. Prof. Msambichaka amewahi kuwa Mwenyekiti wa Bodi wa mashirika kadhaa ikiwepo Bodi ya Wakurugenzi ya Ngozi Morogoro, Taasisi ya Fedha ya Maendeleo ya Biashara, Mfuko wa Bima ya Afya ya Taifa, Chuo Kikuu cha Biashara Moshi (MUCCOBS), Usajili wa Biashara na Utoaji wa Leseni  [BRELA], Mamlaka ya Maendeleo ya Bonde la Mto Rufiji (RUBADA), Chuo cha Ustawi wa Jamill na Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC).

Bwana Joseph Matanga Kahungwa – Mtanzania

Mjumbe

Bwana Kahungwa ana shahada ya Biashara katika masuala ya Uhasibu kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, 1987, na shahada ya Uzamili katika Uongozi wa Biashara kutoka Chuo Kikuu cha Dar-es-Salaam, 2003. Pia yeye ni Makamu wa Rais (Kilimo) wa TCCIA tangu Mei 2013 mpaka sasa, mwanahisa na mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Kampuni ya Uwekezaji ya TCCIA na pia Mwenyekiti wa Kamati ya Ukaguzi. Bwana Kahungwa alikuwa Mwenyekiti wa TCCIA Mkoa wa Mwanza (Machi 2008 hadi Machi 2013). Hali kadhalika, alikuwa Makamu Mwenyekiti wa TCCIA Mkoa wa Mwanza (Machi 2001 hadi Machi 2008), Mjumbe wa Bodi ya CRDB Bank PLC kutoka mwaka 2001 hadi 2006, Mjumbe wa Kamati ya Fedha ya Kanisa la Africa Inland Church Tanzania (AICT) kutoka 1977 hadi 2014. Awali, alikuwa na nyadhifa kama vile Meneja Uhusiano wa Kampuni ya Pangea Minerals Ltd kutoka Julai 1999 hadi 2001, Mhasibu Mwandamizi - Pangea Minerals Ltd, Mhasibu Mwandamizi na Msimamizi wa Mikopo – Bodi ya Biashara ya Nje kutoka 1992 hadi 1994. Pia alikuwa Mhasibu wa Bodi hiyo kutoka 1991 hadi 1992. Amesajiliwa na na Chuo cha Wakurugenzi Tanzania (IoDT).

Bwana Peter W. Kifunguomali – Mtanzania

Afisa Mtendaji Mkuu/ Katibu wa Bodi

Ndugu Kifunguomali ana Shahada ya Uzamili katika masuala ya Biashara ya Kimataifa kutoka Chuo Kikuu cha  Jamia Millia Islamia, New Delhi, mwaka 2014 na Shahada ya Sayansi ya Uchumi katika kubuni Miradi na kuisimamia kutoka Chuo Kikuu cha Mzumbe mwaka 2007. Aliwahi kufanya kazi katika Wizara ya Mali Asili na Utalii, Benki ya NBC na Mfuko wa LAPF. Kabla ya wadhifa wake wa sasa kwenye Kampuni, alikuwa Mkuu wa Kitengo cha Mipango cha Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa Watumishi wa Umma (PSSSF) tangu Septemba, 2018. Alikuwa ni Mjumbe wa Bodi ya Kampuni toka Julai 2017 hadi June, 2019.

Valentino Maganga Daudi

Board Member

Valentino Maganga Daudi is a distinguished legal expert with over 15 years of experience in corporate law, social security, labour, taxation, investment, and international trade and finance law.

He is a registered Advocate of the High Court of Tanzania and holds an LL.B (Hons) and an LL.M from the University of Dar es Salaam. As a certified Director and Board Secretary by the Institute of Directors of Tanzania (IoDT), Mr Maganga currently serves as Principal Legal Counsel at the Public Service Social Security Fund (PSSSF). He is also a member of the Labour, Social, and Economic Council (LESCO) and acts as an Advisory Board Member of the Global Alliance for Legal Aid (USA). Additionally, he serves on the boards of Mwanza City Commercial Complex Co. Ltd (Rock City Mall) and TCCIA Investment PLC.

He played a pivotal role in drafting the Portability of Social Security Benefits Framework for SADC countries and collaborated with the ILO and World Bank on extending social protection for migrant workers in Africa. A respected legal scholar, he has authored and presented several papers on critical legal and policy issues.

With his extensive expertise in governance and regulatory frameworks, Mr Maganga brings valuable strategic insight to Afriprise Investments PLC.

Vicent Bruno Minja

Board Member

Vicent Bruno Minja is a seasoned business leader with extensive experience across various industries. As the President of the Tanzania Chamber of Commerce, Industry, and Agriculture (TCCIA), he plays a crucial role in shaping the country's business landscape. He also serves as a Board Member of the East Africa Chamber of Commerce, Industry, and Agriculture and co-chairs the Business Environment Working Group under the Tanzania National Business Council (TNBC).

With a background in finance, business management, and governance, Vicent holds a Master’s degree in International Business from the University of Central England and is a Certified Public Accountant (CPA-T). He also earned a Postgraduate Diploma in Financial Management from the Institute of Finance Management (IFM).

Over the past two decades, he has built and led successful businesses, including Nakiete Pharmacy T Ltd, Misha East Africa Ltd, and Izungo Apartments and Tours Ltd, with ventures in pharmaceuticals, office equipment, construction materials, hospitality, and mining.

As a Board Member of AFRIPRISE Investments PLC, Vicent contributes strategic leadership, financial expertise, and a deep understanding of the investment landscape, aiding the company’s growth and long-term success.

Contact info

TCCIA Investment Company Limited [TICL] is a public limited liability company that was established by shareholders to expand financing sources to participate meaningfully in the ownership and control of the Tanzanian economy